Jinsi ya Kupika Desert ya Ndizi na Chocolate



Desert ya ndizi mbivu, maziwa fresh, chocolate na mkate.. Ni tamu sana sana 

MAHITAJI 


  • Ndizi mbivu 2 
  • Maziwa nusu glasi 
  • Chocolate bar 4 
  • Mkate vipande 4 

KUANDAA MKATE 



  1. Toast mkate wako kisha kata katika vipande kwa shape upendayo 
  2. NDIZI MBIVU - Kata vipande vidogo vigodo kisha zirosti kwa mafuta hadi ziwe rangi ya kahawia kisha kausha na wacha zipoe 
  3.  CHOCOLATE na MAZIWA - Yeyusha chocolate yako ukimix na maziwa ya uvugu vugu  vikiwa vimeyeyuka weka zile ndizi na endelea kusaga saga hadi vilainike kwa pamoja vyote. Sasa anza kupaka mkate wa kwanza chini, kisha weka kwa sahani kila layer unaiwekea huo uji wa chocolate , maziwa na ndizi hadi mwisho kisha weka kwa friji ipoe kidogo na tayari kwa kula. Ni rahisi na ni tamu sana #kudimbamba

No comments:

Post a Comment

@chefkile